Saturday, November 21, 2009


Buster rhymes akihojiwa na vyombo vya habari mjini dar

zamaradi mketema na mwanamuziki wa buster rhymes
Mtangazaji maarufu wa clouds fm bi zamaradi mketema akiwa amepozi na mwanamuziki aliyekuja na buster rhymes

Buster rhymes na crew yake wakiwasili katika hotel ya kilimanjaro leo hii tar 21/11/2009 mjini dar es salaam

BUSTER RHYMES NDANI YA FIESTA DAR


Watangazaji wa clouds fm wakiwa wamepozi na mwanamuziki aliyekuja na buster rhyme kwa ajiri ya fiesta 2009 dar

Sunday, October 25, 2009

Mambo Ya Kuchukua Waume Na Wake za Watu





Ukiwa unapenda raha usisahau kuna karaha pia ndani yake, sasa kama umezoea vya wizi jua ipo siku itakukuta hii kama ambao wana ndoa hawa walivyokosa adabu sasa ona mambo waliyoyapata

MARUBANI WASAHAU KUTUA NDEGE


Wasiwasi mkubwa uliwakumba wana anga wa kimarekani siku ya ijumaa tarehe 23 october pale ambapo ndege ya NWA ilipokosa mawasiliano kwa kipindi cha dakika 78. Ndege hiyo ambayo ilikuwa inatokea San Diego kuelekea Minneapolis na ikiwa imebeba abiria 144.
Pamoja na jitihada za kuwapigia simu na kufanya mawasiliano ya aina yote bila mafanikio iliwafanya Wana Anga wakimarekani kupeleka mawazo yao moja kwa moja kuwa ndege hiyo imetekwa nyara.

"Tulikuwa tukiwaona kwenye radar na kuwazungumzisha ila hatukupata jibu, hilo jambo lilitutia wasiwasi sana hayo" ni maneno ya msemaji mkuu wa wana anga hao mr Toni Molinari.
Imesadikiwa ya kuwa marubani hao walipitiwa na usingizi ndio maana hawakuweza sikia wala kujibu ujumbe wowote uliotumwa kwao.

Thursday, October 22, 2009

WAPENDA VIATU MPOOO? SPECIAL KWA KINA DADA









/>


Hayaa hayaa hayaa shughuli imeingia mvua masheikh wanakula wima. masistadoo si huwa mnadai mnapenda sanaa hills, hivi ni viatu vya pekee hivi mtu ukivaa utajiskiaje???

WAKATI WA SODOMA UMEWADIA





Hii ndo hali ya dunia yetu kwa sasa, matendo ya ajabu na yanazidi kuongezeka, kama unavyoona pichani hapo juu.
Daniel Chege Gichia (kushoto, mwenye ndevu) ambaye ni bibi harusi akiwa na bwana harusi wake Charles Ngengi wakati wa ndoa yao.

Ndoa iliyofungwa hivi karibuni jijini London, Uingereza, kati ya wanaume wawili, raia wa Kenya, Daniel Chege Gichia (mwenye umri wa miaka 39) na Charles Ngengi (40), imezua gumzo kubwa miongoni mwa wananchi nchini Kenya... hali hii inaongezeka sana
kwa kasi sijui tutafika wapi.

Na picha ya chini ni kati ya wanandoa wawili kutoka nchini marekani Bwana Jamil na Bi Michael. oops na Michael aliyeshika maua, ambao pia waliingia katika ulimwengu huu wa sodoma week chache zilizopita. Mungu atuepusha kua miongoni mwao ni kinyume cha mila na desturi zetu.

Saturday, September 19, 2009

EID MUBARAK



Asalaam aleykum warahma tullah taala wabarakat. kwa niaba ya waislam wenzangu ningependa kuwatakia waislam wote duniani Eid njema. Tunaomba Mwenyezi Mungu azikubali funga zetu na sala zetu na atujaalie tuweze kufunga ramadhani zifuatazo. Inshallah

Tuesday, September 15, 2009

MRUSHA VIATU MAARUFU DUNIANI AACHIWA HURU



Mwandishi wa habari ambae alimrushia kiatu rais wa zamani wa marekani bwana G.Bush ameachiwa huru leo, mwandishi huyu ambae anajulikana kwa jina la Muntazer Al Zaid amejipatia umaarufu kwa kitendo chake kinachoitwa cha ushujaa kwa kumrushia rais mstaafu huyo viatu, kwa kile alichosema ni msisitizo wa kutaka wanajeshi wa kimarekani waondoke nchini irak.
Aliachiwa huru tangu jana ila kutokana na kutotimia kwa baadhi ya fomu za kuachiwa huru ikabidi atoke leo, Anasema kuwa alipata mateso mengi sana moja wapo ni kupigwa shoti ya umeme nk. ila anafuraha kwa kuwa huru, na watu wanamuona ni shujaa.

Monday, September 14, 2009

MPAKANJIA AFARIKI DUNIA


Habari zilizotufikia hivi sasa zinasema kuwa MOHAMED MPAKANJIA amefariki dunia! Akithibitisha kifo hicho, jamaa wa karibu wa mfanyabiashara huyo, alisema kuwa Medy amefariki leo mchana katika hospitali ya Lugalo jijini Dar es salaam alikopelekwa jana usiku akitokea kwa Dk Massawe wa Temeke, ambako alikimbizwa kwa huduma ya kwanza. Habari zinasema kuwa Medy, ambaye alikuwa mume wa marehemu Amina Chifupa, hali yake kiafya haikuwa nzuri katika siku za hivi karibuni. MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU PEPONI - AMIN!!!!

Friday, August 28, 2009

HAPPY BIRTHDAY UNCLE MICHUZI






Leo ilikuwa ni siku ya kuzaliwa kwa mkuu Issa Michuzi ambaye aliamua kujumuika pamoja na Wadau mbali mbali waliopo ndani ya jiji la Dar katika Ftari iliyoandaliwa katika mgahawa wa cheifplide pale mtaa wa Libya street,sherehe hiyo ilifana sana tena sana.Blogu hii inampa pongezi sana mzee wa Libeneke kwa kukumbuka siku yake ya kuzaliwa na Mwenyezi Mungu amjaalie afya njema na Maisha marefu Inshaallah.

Friday, August 21, 2009

RAMADHAN NJEMA




Bismillah Rahman Raheem
Ndugu wadau popote pale mlipo napenda kuwatakia mfungowa Ramadhani mwema, wenye baraka na naomba Mwenyezi Mungu atujaalie tuweze kumaliza salama na apokee dua zetu na funga zetu. na kwa yoyote atakaependa kupata nasaha za fadhila za mwezi huu kuna baadhi ya sites anaweza kutembelea akapata mawili matatu ambayo yatamsaidia kukamilisha mwezi huu mtukufu,
http://www.alhidaaya.com
http://www.sw.quran.nu hizi ni baadhi ya website za kiswahili na hii ifuatayo ni ya kiingereza http://www.islamicity.com

Wabillah Tawfiq

HASHEEM HIVI HII NI POZI, MDADI AU UNAJIKUNA????

SWALI LA KIZUSHI HIVI HII TATOO INAMAANISHA NINI?

Thursday, June 25, 2009

MICHAEL JACKSON AFARIKI DUNIA


.

Michael suffered a cardiac arrest earlier this afternoon at his Holmby Hills home and paramedics were unable to revive him. We're told when paramedics arrived Jackson had no pulse and they never got a pulse back.

A source tells us Jackson was dead when paramedics arrived.

Once at the hospital, the staff tried to resuscitate him but he was completely unresponsive.

We're told one of the staff members at Jackson's home called 911.

La Toya ran in the hospital sobbing after Jackson was pronounced dead.

Michael is survived by three children: Michael Joseph Jackson, Jr., Paris Michael Katherine Jackson and Prince "Blanket" Michael Jackson II.

Tuesday, June 23, 2009

BALAA NDANI YA DC





Treni ya abilia imesababisha mauaji mjini dc washington, Treni hiyo inayojulikana kama metro ambayo huwa katika msitari mwekundu na inayofanya safari yake ya kusaidia usafiri kati ka miji ya dc , maryland na virginia, imesababisha mauaji yanayokusudia watu zaidi ya kumi kufa papo hapo na wengine zaidi ya 50 wakiwa majeruhi

Saturday, June 20, 2009

WAMAREKANI KUFUNDISHWA KIINGEREZA ASILIA TOKA AFRIKA


Afisa Mwandamizi wa ubalozi wa Marekani nchini Dr.Tulinabo Mushingi(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na vijana wa vyuo vikuu wanaosomea shahada za kwanza wanaosafiri kesho kwenda Marekani kwa programu ya kufundisha lugha ya kiingereza kwa mataifa ya Afrika. Programu hiyo inagharimiwa na watu wa Marekani,ni programu inayofuzwa kwa kina inayolenga kuongeza usomaji kwa lugha ya kingereza,kuandika,kusoma na kusikiliza maarifa ya wanazuoni wa kiafrika lakini kubwa zaidi ni kuwapa uelewa mpana zaidi wa tamaduni za kimarekani pamoja na mila na desturi zao.

KUMEKUCHA TANZANIA MAMBO YA UCHAGUZI


Mgombea wa CCM Oscar Rwegasira Mukasa akijinadi wa wapiga kura katika Kijiji cha Mavota wilaya Biharamulo katika moja ya mikutano ya CCM ya kampeni kuwania kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Biharamulo Magharibi.Picha na Frederick Katulanda

RUBANI AFARIKI NDEGE IKIWA ANGANI, WATU WAOMBA SALA ZAO ZA MWISHO


Katika kisa ambacho wengi watadhani ni muujiza, abiria 247 waliokuwa wakisafiri na ndege ya kampuni ya Continental kutoka Ubelgiji hadi Marekani waliponea chupuchupu wakati nahodha wa ndege yao alipofariki dunia.
Msemaji wa Halmashauri inayosimamia usafiri wa ndege Marekani, Arlene Salac alisema kulikuwa na marubani wengine wawili ambao waliidhibiti ndege hiyo aina ya Boeing 777 hadi uwanja wa ndege wa Newark Liberty ambako ilitua kwa dharura.

Mtaalamu mmoja wa usafiri wa ndege, Jim Ferguson alisema si jambo la kawaida rubani kufariki dunia akiwa angani.

Kwa kawaida ndege hiyo huendeshwa na marubani wawili. Lakini kwa bahati nzuri wakati huu, kulikuwa na mwingine wa ziada.

Bwana Ferguson alisema ingekuwa vigumu kwa rubani mmoja kuidhibiti ndege hiyo kutua.

Abiria hawakuambiwa lolote kuhusu mkasa huo. Miongoni mwao alikuwa daktari mmoja wa maswala ya moyo, Dr. Julien Struyven ambaye aliitikia tangazo daktari yeyote kwenye ndege hiyo kujitokeza.

Abiria hawakujua kwamba mwito ulitolewa kwa ajili ya kumuokoa rubani wa ndege hiyo.

Dr Struyven alipomfikia rubani huyo alikuta kama tayari ameaga dunia.

“Hakukuwa na uwezekano wowote wa kumwokoa,” alisema Dr Struyven.

Alisema huenda rubani huyo mwenye umri wa miaka 60 na ambaye amehudumia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 20 alifariki dunia kutokana na matatizo ya moyo

WAZIRI WA ULINZI NCHINI SOMALIA AUWAWA


Waziri wa usalama wa ndani wa Somalia Omar Hashi Aden ameuwawa kwenye shambulio la kujitoa muhanga la bomu lililotegwa kwenye gari kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Watu wengine zaidi ya 20 wameuwawa kwenye mlipuko huo katika Hoteli ya Beledweyne, kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.

Miongoni mwa waliouwawa ni maafisa kadhaa wa Kidiplomasia wa Somalia.

Rais wa Somalia Sheikh Sharif Sheikh Ahmed amelaumu kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Al-Shabaab , ambalo pia baadaye lilikiri kufanya shambulio hilo.

Kundi hilo linaaminika kuwa na uhusiano na mtandao wa kigaidi wa Al -Qaeda.

Siku ya jumaatano watu 10 walikufa wakati kombora liliporushwa kwenye msikiti mjini Mogadishu.

Katika shambulizi la Alhamisi , walioshuhudia walisema mlipuaji wa kujitoa muhanga alilipua gari lililojaa mabomu kwenye hoteli ya Medina , mjini Beledweyne, yapata Kilomita 400 kaskazini mwa Mogadishu.

Abdulkarim Ibrahim Lakanyo, balozi wa zamani wa Somalia nchini Ethiopia pia ameripotiwa kuwa miongoni mwa waliouwawa.

Mwandishi wa BBC Will Ross anasema bwana Aden alihamia mjini Beledweyne hivi majuzi, mji ulioko karibu na mpaka wa Ethiopia, katika jitihada za kukomesha wanamgambo wa Kiislamu wasiendelee kuthibiti maeneo mengi zaidi.

Rais Ahmed ameambia mkutano wa waandishi wa habari mjini Mogadishu kwamba Somalia imevamiwa na magaidi wasiotaka kuona benderea ya nchi hiyo, wala amani .

Amesema kundi hilo la Al- shabaab linajificha kwenye Uislamu kuendesha ukatili wao.

Somalia haijawa na serikali dhabiti tangu mwaka wa 1991 , na zaidi ya watu milioni nne , ambao ni asilimia 75 ya raia wa nchi hiyo wanahitaji msaada wa chakula.

Kundi la Al- Shabaab ni mshirika katika muungano wa wanamgambo wa kiislamu wenye msimamo mkali ambao wamekuwa wakijaribu kuiangusha serikali ya mpito ya Somalia inayoungwa mkono na umoja wa mataifa.

Rais Ahmed , ambaye mwenyewe ni muislamu mwenye msimamo wa wastani alichukua khatamu nchini Somalia mwezi Januari , lakini hata baada ya kuanzisha utawala wa kuzingatia sheria za kiislamu , hatua hiyo bado haijawaridhisha wapiganaji hao.

Jumaatano , kamanda mkuu wa Polisi mjini Mogadishu aliuwawa kwenye mashambulizi dhidi ya ngome za wanamgambo.

Mwakilishi wa shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR nchini Somalia amesema umwagikaji damu wa hivi karibuni nchini Somalia ndio mbaya zaidi kuikumba nchi hiyo kwa muda wa karibu miaka 20.

OBAMA KUFANYA MABADILIKO YA UCHUMI NCHINI MAREKANI


Mfumo huu mpya unalenga kuilinda Marekani kukumbwa na mzozo wa kuichumi sawa na ulio sasa katika siku za usoni.

Rais wa marekani Barack Obama amependekeza kuufanyia mabadiliko makubwa mfumo wa uchumi wa marekani pamoja na njia ambazo zinaweza kuzuia mzozo mbaya wa kiuchumi kama ule uliopo sasa duniani kujirudia tena.

Waziri wa fedha nchini Marekani Timothy Geithner anatarajiwa kuwasilisha mpango wa mabadiliko ya mfumo wa uchumi wa Marekani katika bunge hii leo pamoja na kwenye kamati inayohusika na maswala ya fedha katika bunge la Marekani.

Mpango huo wa rais Obama una lengo la kuipa mamlaka benki kuu nchini Marekani, ili kusimamia masuala yote ya kifedha na kuunda mbinu ambazo zinaweza kuzuia kuwepo tena kwa vyanzo vilivyo sababisha kutokea kwa mzozo wa kiuchumi uliopo sasa.

Wadadisi wanasema kuwa mabadiliko hayo yaliyopendekezwa na rais Obama ni muhimu hasa kwa masoko yanayokabiliwa na matatizo lakini pia huenda yakawa vigumu kutekelezwa.

Akiuanzisha mpango huo jana jumatano rais Obama alisema kuwa hayo ndio mabadiliko makubwa zaidi tangu mwaka 1930, yaliyo na lengo la kuzuia kuporomoka kwa mifumo ya kifedha ambayo mara nyingi hutokana na kuwepo kwa madeni.

Hata hivyo kuna baadhi ya wanaoukosoa mpango huo wakisema kuwa, hautafanikiwa vile inayohitajika huku wengine wakisema kuwa serikali itakuwa na ushawishi mkubwa juu ya sekta za kibinafsi.

Kati ya mapendekezo kwenye mpango huo ni pamoja na kuipa benki kuu madaraka ya kuingilia kati mifumo ya uchumi ambayo inaonekana kuhatarisha uchumi ikiwemo ile ambayo haimiliki mabenki.

Hatua hizi ni muhimu na zinahitajika, lakini zinakosa mabadiliko makuu ambayo yangesaidia katika kutimiza malengo haya, alisema Douglas Elliot mwana uchumi mmoja katika taasisi moja nchini Marekani.

Mwana uchumi huyo alisema kuwa pia kunahitajiwa kufanyika mabadiliko katika makampuni makubwa, ambayo yanaweza kusababisha kuyumba kwa uchumi na pia na kuwalinda wananchi kiuchumi, matamshi ambayo pia yalitolewa na kundi linalowajumuisha wafanibiashara pamoja na wasomi lililobuniwa mwaka 2006.

Mpango huo unatajwa kulenga moja kwa moja masuala muhimu pamoja na mabadiliko makubwa na kuweka mikakati ya kukabiliana na masula yaliyochangia kutokea kwa mzozo uliopo sasa.

Hata hivo wengi wameukosoa mpango kuwa kuwa mkali, ambao huenda ukazuia uwekezaji katika mifumo ya uchumi. Wanasema kuwa mpango huo utalegeza huduma zinazotolewa na mifumo ya kuichumi na kutoa uishindani kati ya makampuni makubwa na yale ambayo bado ni madogo.

Hali kadhalika kuna wasi wasi, kwa wale wanaoutaja mpango huo kama ulio mkubwa mno, na huenda ukawa vigumu kuutekeleza na vile vile ukatoa hali ya kutokuwepo kwa utabiri katika siku za mbeleni kwenye masoko ya kifedha na katika badhii ya mifumo ya uchumi.

SHIRIKA LA AL LAONYA KUWA MATESO BADO YAPO ZIMBAMWE


Shirika la Kutetea Haki za binadamu Amnesty International limeilaumu serikali ya Zimbabwe kwa kuendelea kuhusika na vitendo vya mateso yanayokiuka haki za binadamu.Taarifa hiyo ilitolewa na Katibu Mkuu wa Shirika hilo Irene Khan aliyefanya mkutano na waandishi wa habari baada ya kukamilisha ziara ya siku 6 nchini Zimbabwe.

Kulingana na Bibi Khan visa vya ghasia zilizo na misingi ya kisiasa vimepungua ikilinganishwa na mwaka mmoja uliopita lakini bado vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu vinaendelea kutokea.Kauli hizo zimetolewa wakati ambapo wawakilishi wa Umoja wa Ulaya na Zimbabwe wamefanya mazungumzo rasmi ya kwanza katika kipindi cha miaka 7 iliyopita.Kamishna wa masuala ya misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Ulaya Louis Michel aliyezungumza na waandishi wa habari mjini Brussels baada ya kukutana na Waziri Mkuu wa Zimbabwe Morgan Tsvangirai alisema kuwa Umoja huo una azma ya kurejesha uhusiano kati yao baada ya kutatua baadhi ya masuala yanayozua mitazamo tofauti.

WAANDISHI WA HABARI MARUFUKU KUTANGAZA BEI ZA VIUNGO VYA ALBINO VINACHOCHEA MAUAJI YAO NCHINI TANZANIA


Na Sharon Sauwa
Washiriki wa mkutano wa kujadili mauaji ya albino, wamevitaka vyombo vya habari kutotangaza bei ya viungo vya walemavu hao.
Wamesema kufanya hivyo kunachangia kuhamasisha mauaji ya albino kwa kuwashawishi watu kufanya biashara ya namna hiyo.

Walitoa ushauri huo walipokuwa wakiwasilisha majadiliano ya vikundi jijini Dar es Salaam jana.

Hali kadhalika, wameitaka serikali kuweka wakaguzi katika maduka ya kuuza dawa za asili kama wafanyavyo katika maduka ya dawa za viwandani.

Walisema kuwa kufanya hivyo kutawawezesha kubaini iwapo dawa wanazouza haziendi kinyume na kanuni na sheria za nchi.

"Kwenye maduka haya asiyekuwa na ujuzi wa dawa za kienyeji, anauza tu ama dereva teksi anaweza naye leo hii akafungua duka la dawa za asili na anakubalika," alisema mmoja wa washiriki wa semina hiyo, Rose Abdallah.

Walisema hakuna watu wanaofahamu kinachouzwa katika maduka hayo hali inayowafanya baadhi yao kuuza viungo vya wanyama wakidai kuwa vinatumika katika kuponya magonjwa mbalimbali.

ABDALLAH MOHAMED ALI (2009)


Akijaribu kupanga mikakati juu ya uongozi wake mpya mwaka 2009

HUYU NDIO MWENYEKITI MPYA WA WATANZANIA NCHINI GREECE


Si mwingine ni ndugu yetu ABDALLAH MOHAMED ALI

WATANZANIA WAISHIO MJINI ATHENS NCHINI GREECE WAFANYA UCHAGUZI WA VIONGOZI


Kiutendaji, jumuiya hii ilikuwa ikiendelezwa na watu wachache waliokuwa na moyo na upendo wa kuona umoja wa watanzania unaendelea na kudumu. Watu hao baada ya kugundua kwamba muda muwafaka wa kufanya uchaguzi umewadia, na kwamba watu wanahitaji mabadiliko, walikubaliana kwa pamoja zitafutwe mbinu zitazohakikisha ufanikishaji wa uchaguzi.


Na hapo ndipo zilipoanza kampeni za uchaguzi, ambao ulifanyika katika ukumbi wa Sieraleone siku ya Jumamosi 07/03/2009 kuanzia saa moja usiku hadi saa tisa.Ulikuwa ni uchaguzi ULIOFANA na wa HAKI. Takriban watanzania wote walihudhuria, hata wale ambao siku za nyuma walikuwa hawana hamasa kabisa na jumuiya.Kulikuwa na kila aina ya viburudisho, vilivyosindikizwa na na mziki wa kupendeza .

Katika uchaguzi huu walichaguliwa viongozi wapya wafuatao:


MWENYEKITI
ABDALLA MOHAMED ALI. (AMASHA)

MAKAMU M/KITI
SALUM FRANCIS WILLIAM. (Mzee FRANCIS.)

KATIBU MKUU
KAYU ALLY LIGOPORA. (KAYU)

KATIBU MSAIDIZI
MUNGI HUSSEIN SALUM. ( MUNGI)
MWEKA HAZINA
AZIZI ALI. ( AZIZI )

NAIBU MWEKA HAZINA
CHINA SELEMAN HASSAN. (CHINA)

AFISA WA JAMII
ALLY MOHAMMED UBAO. ( ALI UBAO)


WAJUMBE WA KAMATI :
1 ALLY SALUM NYAU. ( ALI NYAU )
2 MWANSITI ISSA MNTAMBO. ( MWASITI )
3. MWAMVITA HATIBU MAKENGA ( MACHO )

ZE UTAMU CHINI YA ULINZI, WATANZANIA MNASEMAJE???



Polisi wa Tanzania kwa kushirikiana na Polisi wa Kimataifa (Interpol),wamefanikiwa kumshika Raia mmoja wa Uingereza ambaye ana asili ya Tanzania Ndg Malecela Peter Lusinde (pichani juu) mwenye umri wa miaka 39 na kutuhumiwa kwa kuundesha mtandao wa Ze Utamu.Ndugu Malecela ambaye anajulikana pia kwa jina la "Male" ni Mtaalamu wa kompyuta na ana uwezo wa kuzungumza na kuandika Kiingereza,kiswahili na kichina ana makazi katika mji wa Essex nchini Uingereza.

Wataalamu wa Idara ya upelelezi kutoka Tanzania wakishirikiana na wenzao wa Uingereza wamefanikiwa kuonana na Ndg Male na kupata ushahidi wa kutosha kwamba ndiye alikuwa mmiliki wa Mtandao huo.Idara ya Upelelezi na polisi wa Uingereza wameutaarifu Ubalozi wa Tanzania mjini London kuhusu suala hilo.Maofisa Ubalozi Mr.Clement Kiondo na Amos Msanjila wamefahamishwa jambo hilo.Malecela ni Mtoto wa Mzee Job Lusinde ambaye amewahi kufanya kazi kwenye nyadhifa mbalimbali za utumishi wa serikali Nchini Tanzania.

Habari zilizothibitishwa zinadai kuwa Ndg Malecela amerudishwa Tanzania kwenda kujibu tuhuma mbalimbali za kuendesha mtandao uliokuwa unadhalilisha watu,kuna malalamiko 6850 yaliyoandikishwa kulaumu udhalilishwaji wa watu uliofanywa na mtandao huo,Mtandao huo ulisimamishwa mwanzoni mwa mwezi wa pili kwa maombi ya serikali ya Tanzania baada ya kutoa picha ya kumdhalilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete,ufuatiliaji uliofanywa baada ya picha hiyo ndio umepelekea kukamatwa kwa Ndg Malecela.

Haijaeleweka wazi Ndg Malecela atashitakiwa kwa sheria gani? Lakini ni wazi kwamba atashitakiwa Nchini Tanzania.Licha ya Ndg. Malecela Polisi wa Upelelezi wamezungumza na Watanzania wengine wawili katika miji ya Wichita na San Diego Nchini Marekani,ambao pia wanahusishwa na Mtandao huo wa Ze Utamu.

CHIKU NA NINDI HAWAKO NYUMA , MWANAMKE KULA!!!

AMANI KHERI AKIWA ANATAMBA KATIKA BANDA LA KWAO LA KITANZANIA

MAMBO YA MAONESHO YA SANAA MJINI ATHENS GREECE HAYO

SALAMU ZA BONGO SIKU HIZI KAMA MAMTONI TUU!!!


Mheshimiwa Ndasa..
Pichani ni Mbunge wa Sumvwe,Richard Ndasa CCM (Kushoto)akisalimiana na Mbunge
wa Chadema Lucy Owenya kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma

USHURU SASA NJEE KWA VYOMBO VYA DINI


Wiki moja baada ya serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kutangaza kuanza kutoza ushuru kwa mashirika yote ya Dini wakati ikiwasilisha bajeti ya Mwaka 2009/10 bungeni mjini Dodoma na kuzua maswali mengi kutoka kwa Wabunge Leo Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mizengo Kayanza Pinda ametangaza Rasmi kufuta ushuru Kwa madhehebu yote ya Dini na huo na kurejea kama Mwanzo.Mheshimiwa Waziri Mkuu ametangaza Uamuzi huo Mjini Dodoma Hivi Leo

Shavu kwa Rais Jakaya Kikwete Kutoka chicago bulls

MAMBO YA KIKWETE KATIKA KIKAPU


Pichani ni jezi na mpira wenye saini za wachezaji wa timu ya Chicago Bulls ya nchini Marekani.Zawadi hizo alipewa Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete alipokuwa ziarani Marekani hivi karibuni.Rais Jakaya Kikwete alipata kucheza mpira wa vikapu.Pichani kulia ni mwandishi wa Rais Msaidizi,Premmy Kibanga akizionyesha jezi hizo kwa waandishi wa Habari na Kushoto ni mwandishi wa Habri wa kituo cha channel 5 cha jijini Dar es Salaam BW Patric.