Wednesday, May 13, 2009

HAYA AMINI HUSIAMINI


Katika hara ya kushangaza watu wengiii yule mwana dada rihanna ambaye alikuwa kapewa kibano na chris brown,inasemekana kuwa ana mtindo wa kupiga picha za uchi, na sasa zimeshanyakwa na makachero, na ziko hewani kwa internate,
sasa angalia sura hii ilivyo nzuri kabla ya ugomvi na jamaa yake

USISHANGAE HII NI SURA HALISI YA RIHANNA


katika hari isiyokuwa ya kawaida rihhana alijikuta akila makofi kutoka kwa mpenzi wake chriss brown , kwa kile inachodaiwa kuwa amemuambukiza ugonjwa wa zinaa unaotokana na kujaamiana, na hapa ndio anavyoonekana baada ya kukatwa makofi,

Saturday, May 9, 2009

JACOB ZUMA RAIS MPYA WA AFRIKA KUSINI

Capetown, Bunge la south afrika limemtangaza Jacob Zuma kuwa ni rais wa nne wa nchi hiyo. Zuma ambae ametokea kwenye chama cha ANC (African National Congress) alipata jumla ya asilimia 66 za kura zilizopigwa. Sherehe ya kutawazwa kwake imehudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo viongozi wa kimataifa wapatao 30 akiwemo rais Robert Mugabe na kiongozi wa libia Muammar al Gaddaf.

Wednesday, May 6, 2009

MAFURIKO YAUA 30 BRASIL


Watu 30 wamekufa na wengine 180,000 kupoteza nyumba na mali zao baada ya mvua kubwa iliyonyesha na kusababisha mafuriko makubwa kusini mwa nchi ya brasil. Miji isiyopungua sita imeathirika kwa mafuriko haya na watu wanakosa misaada kwa kuwa barabara zote zimesombwa na kufunikwa na maji. Serikali ya Brasil inasema itajitahidi kadri iwezavyo kuokoa wanachi wake wote kwenye janga hili.

WAZIRI MKUU WA KENYA RAILA ODINGA ABATIZWA

Baadhi ya watani wetu wa jadi (Wakenya) jana walipokea ubatizo wa Waziri Mkuu Raila Odinga kwa hisia tofauti baada ya kudhihirika hakubadili jina lake, Bw Odinga alibatizwa na Askofu David Owuor wa kanisa la Holiness and Repentance Ministries mnamo jumatatu jioni, Bwana Odinga alionekana amevalia kanzu nyeupe kama ya kiislam, lakini kilichoshangaza watu wengi ni kwamba kinyume na watu wengine wanapobatizwa, Odinga ataendelea kutumia majina yake ya Raila Amolo Odinga kama kawaida.

Tuesday, May 5, 2009

BIBI NA BWANA HARUSI WAUWAWA KWENYE SHEREHE YA HARUSI YAO

Huyu ni mmoja wa majeruhi waliojeruhiwa vibaya kwa risasi na bomu huko nchini Uturuki, baada ya watu wawili waliovaa vinyago usoni kuingia ukumbini kwenye sherehe ya harusi iliyofanyika kitongoji cha Bilge Koyu (2okm) kutoka mji wa Mardin na kufyatua risasi mfululizo na kurusha bomu na kusababisha vifo vya watu 44 wakiwemo bibi na bwana harusi siku ya jumatatu jioni . Sababu kubwa ni kwanini bibi harusi aolewe na mtu wa kabila lingine,

Friday, May 1, 2009

"Netherlands Queens Day Drama" Badala ya sherehe ni msiba








Tarehe 30 ya mwezi wa April kila mwaka ni siku ya kuzaliwa kwa malkia wa uholanzi, hii ni sikuuu kwa wananchi na wakazi wa uholanzi, Mwaka 2009 umekuwa ni siku ya wa majonzi kwa taifa la uholanzi baada ya Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Karst T. mwenye umri wa miaka 38 alipovamia umati wa watu waliokuwa wakimshangilia malkia na familia yake na kuwagonga na gari alilokuwa akiendesha na kusababisha vifo vya watu 7 na kujeruhi 14 katika mji wa Apeldoorn ambapo sherehe hiyo ilifanyika rasmi, mtuhumiwa alifariki muda mchache baada ya tukio. Mungu awapumzishe marehemu kwa amani.









Monday, April 27, 2009

KWANI WAO WAWEZE WANA NINI HATA MIMI NISHINDWE NINA NINI???




Hayo sio maneno yangu ndugu wadau ni maneno ya Bibi Bette Calman kutoka nchini Australia mwenye umri wa miaka 83 ameuonyesha ulimwengu kuwa hata kama ana umri mkubwa unaweza kuumudu mwili wake.. Bibi huyu anayejipenda kimavazi huwaacha watu midomo wazi kwa uwezo wake wa kupiga push ups na kujipindapinda uwezo pamoja na kuwa na umri huo ambao wazee wengi wa umri wake hawawezi na hulalamikia maumivu ya viungo vyao kwa kisingizio cha umri . Bibi huyu ni mwalimu wa yoga na anayoyafanya hata baadhi ya vijana wengi hatuwezi kuyafanya..pengine hata wewe unayeisoma habari hii huwezi kufanya nadanganya??
Kama unabisha naomba upige push ups ishirini tuone utakavyo kosa kupumua kwa amani, Jamani vijana wenzangu mazoezi ni muhimu sana.

KWANI WAO WAWEZE WANA NINI HATA MIMI NISHINDWE NINA NINI????



Saturday, April 18, 2009

BONGO IKO JUU!!!



Haya ndugu wapendwa mambo ndo hayo kwa wale wanaopenda kujirusha, Kituo kipya cha maraha cha Savannah Lounge & Bar kimefunguliwa rasmi leo katika hotel ya Paradise City ambayo ipo katika jengo la Benjamin Mkapa Tower mtaa wa Azikiwe Avenue opposite na posta mpya. kazi kwenu wadau

BONGO IKO JUU






Saturday, April 11, 2009

OBAMA KATIKA MAISHA YAKE KABLA YA URAISI JE UNAYAJUA?





























Hahaha, haya ndio maisha aliyokuwa nayo rais wa marekani wa sasa Barack Hussein Obama, haya jamani angalieni wenyewe

Thursday, April 9, 2009

vitu hadimu jamani kula raha


JAMANI DC KUNA MAMBO, WATU KUPINDA MGONGO NI KAMA KAWAIDA

Hawa ni wadada wa Tanzania waishio mjini DC Washington, wakiwa katika swala zima la kukonga nyoyo zao, katika style ya kipekee ile ipendwayo na watu wengi kabisa ya pinda mugongo, haya sasa jamani kazi ipo hapo,

SHEIKH YAHYA HUSSEIN BADO ANADAI


Sheikh yahya hussein anasema bado yuko hai na anaendela vizuri tuu, hayo aliyasema akiwa nyumbani kwake mara tuu alipoongea na waandishi wetu wa habari, pembeni yake ni mkewe bi fetty,

Tuesday, April 7, 2009

RAMANI MPYA YA JIJI LA DAR ES SALAAM


Hii ndio ramani mpya ya jiji la dar es salaam tanzania, ambayo inatarajiwa kuanzwa kushugulikiwa haraka iwezekanavyo baada ya pesa za epa kurejeshwa zote, Imekuwa ni ndoto ya kila mtanzania kutaka kuona mji mpya wa dar es salaam ukijengwa upya na kuwa wa kisasa kama ramani yake inavyoonekana juu pichani,

Monday, April 6, 2009

TETEMEKO LA ARDHI LAUA WATU ITALY







Katika hali isiyo tegemewa nchini italy yametokea maafa makubwa yaliyosababishwa na tetemeko la ardhi na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 270, watu wengine zaidi ya kumi elfu kukosa mahali pa kushi na zaidi ya 1500 wakiwa majeruhi, tukio hilo lilitokea alfajiri ya mapema ya jumanne tarehe 7 april huko mjini L'Aquila.




Sunday, April 5, 2009

pepeta pepeta hao

haya jamani semeni wenyewe, hapa kuna kukwepa ngoma jamani?

JAMANI RAHA!! MZUKA WA TAARABU UKIPANDA, WAKUUTULIZA NI MPIGA KINANDA TU


Mashabiki wa muziki wa taarabu wakiwa wamepandisha mzuka hapa hawaambiwi wala hawasikii labda mpaka kinanda kizimwe, kama wenyewe wasemavyo mdadi wa mcheza taarabu wakuutuliza mpiga Kinanda

NYIE AKINA KAKA INAMAANA HAMNIONIII AU ND'O MMEWAFUATA NANIIHI


Mwanadada huyu pichani (kulia) akikata nyonga si kawaida huku akina kaka ambao mara nyingi hutokwa na udenda, wanapoona nyonga za akina dada zikikatwa, wakijifanya kuwa biiize kama kuna kitu kingine wamefuata tofauti na nyonga za akina dada hao

DUUH HAYA MAKUBWA, TAARABU ZA SIKU HIZI BWANA, MIDUME TUPU


Wakati wote ukumbini hapo midume ndio iliyokuwa ikionekana kukata nyonga, kama inavyoonekana pichani wakati muimbaji wa kundi hilo mwanadada, Isha Makongo 'Mashauzi' aliyesimama (katikati) akiimba. Siku hizi kwenye taarabu, wanawake ndio wamekuwa watazamaji wa nyonga za akina kaka zikifanya kazi.

MAMBO YA TAARABU SI MCHEZO


Kundi la Jahazi Modern Taarabu, usiku wa kuamkia leo lilifanya makamuzi 'ya kufa mtu' katika Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi wa kundi hilo Mzee Yusuph, akiwapelekesha puta mashabiki wa kundi hilo (hawapo pichani) kwa kibao cha VIP.

MUNENE NA MUNENE , MWEUSI NA MWEUSI ..., ANATEREEEZA


Bendi ya muziki wa dansi ya Diamond Muzika usiku wa kuamkia leo ilifanya vitu vyake katika Ukumbi wa Mango Garden, ulipo Kinondoni Jijini Dar es Salaam, kama anavyoonekana pichani muimbaji wa bendi hiyo Hassan River (katikati) akilishambulia jukwaa pamoja na wanenguaji wa bendi hiyo.

Saturday, April 4, 2009

Sio swala la utani , ni kweli imekuwa


pichani mama salma kikwete , mke wa Rais wa awamu ya nne ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, mama Salma kikwete akisaidia kumsukumia mkazi wa Dar es salaam kiti bi Rehema nditi ambaye ana matatizo ya mguu na mkono, pembeni yao anayetazama ni mtoto pekee wa bi nditi mwenye miaka 24 anayeitwa maliki, mungu ashukuliwe

Haya maisha bado ni kawaida kwa mtanzania


Huwezi amini katika maisha ya mtanzania bado ni kitendawili katika swala zima la sekta ya miundombinu, siku mvua inaponyesha basi inakuwa ni kama kiyama kwa mtanzania , bara bara zinafurika , foleni haziishi, na hata maji taka hayana pa kwenda, je lini tutafika jamani namna hii.

Muheshimiwa kikwete naye si haba sasa anaweza kuwa alhaji muda wowote

Mheshimiwa kikwete akiwa na baadhi ya wazee wenzake wanaotawala naye nchi , Seif shariff hamad pamoja na mheshimiwa Abraham lipumba, mala baada ya kutokea katikahoteli ya lamada jijini Dar es salaam ilipokuwa ikifanyika ibada ya dua ya kumuombea Shekhe Shaaban khamis Mloo